SIMBACHAWENE AWAONYA WATUMISHI WANAOGUSHI UHAMISHO
Na Nasra Ismail, Geita

Akizungumza na watumishi wa serikali katika halmashauri ya mji wa Geita Waziri wa nchi Ofisi ya Raisi Utumishi wa Umma na Utawala bora George Simbachawene alisema kuwa waliofanya udanganyifu tayari wameshajulikana na wanasubiri kuchukuliwa hatua.
Simbachawene aliongeza kuwa watumishi wengi wana uhamisho ambao ni wa uongo na utapeli na pia wameupata kwa kutoa rushwa.
Aidha Simbachawene aliwaasa watumishi ambao wamefanya udanganyifu ili kupata uhamisho warudi walikotoka kwani wasipofanya hivyo watafukuzwa kazi.
“tukigundua tutawarejesha walikotoka, na kwa maneno haya nayosema yule ambaye alihama kwa uhamisho wa uongo uongo na ameshindwa kuhamisha mshahara wake navoongea hapa arudi alikotoka vinginevyo atafukuzwa kazi” alisema Simbachawene.
Post a Comment