JINSI SAMIA ANAVYOIBADILISHA PWANI KUWA KITOVU KIPYA CHA UCHUMI TANZANIA
Uwepo wa viwanda umekuwa kichocheo muhimu cha ukuaji wa uchumi kwa kuongeza vyanzo vya mapato kwa Serikali za Mitaa na Serikali Kuu kupitia Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA).
Hadi kufikia Machi 2026, Mkoa wa Pwani ulikadiria kukusanya Sh bilioni 189.645 kutoka kodi za ndani na forodha, lakini ulifanikiwa kukusanya Sh bilioni 216.029 sawa na asilimia 113.91 ya lengo.
Kadhalika, Mkoa wa Pwani ulilenga kukusanya Sh bilioni 88 za mapato ya ndani, lakini kufikia Aprili 2026 makusanyo yalikuwa yamefikia bilioni 94 huku hadi Mei yakifikia bilioni 114.5.
Mafanikio hayo ni sehemu ya utekelezaji wa Ilani ya Chama Cha Mapinduzi ya mwaka 2025/2030, yakionyesha usimamizi madhubuti wa Serikali katika kuimarisha uwekezaji, viwanda, bandari, barabara, umeme na miundombinu mingine, ambayo imeendelea kuchochea ukuaji wa uchumi na kuleta maendeleo.
.jpeg)


.jpeg)
.jpeg)
.jpeg)

Post a Comment